Kozi hii inachunguza uundaji wa maneno, mpangilio, kanuni na mahusiano ya maneno katika sentensi ya lugha. Vipengele
muhimu vitakavyochunguzwa vitatokana na mofolojia na sintaksia. Kozi hii basi, inatoa maelezo ya kimsingi kuhusu
dhana ya mofolojia na sintaksia ya Kiswahili. Kwa hiyo, kozi hii inazamia kufafanua dhana za kimsingi za mofolojia na
sintaksia kama vile: mofu, mofimu, alomofu, maneno, uambishaji, uundaji maneno,
uainishaji wa ngeli kimofolojia na kisintaksia.
- Teacher: Hellen Barno